Thiago Motta ameibuka kuwa kipenzi kipya cha Paris Saint-Germain na Bologna wanaripotiwa kukata tamaa juu ya nafasi yao ya kumbakisha Mtaliano huyo mwenye asili ya Brazil.

Miamba hao wa Ligue 1 wameamua kuachana na Christophe Galtier na wamekuwa wakitafuta mbadala wake kwa wiki kadhaa sasa. Julian Nagelsmann alionekana kuwa mmoja wa chaguo lao kuu lakini Mjerumani huyo aliripotiwa kukataa nia yao, na kuwalazimisha kutafuta mahali pengine.
Motta alichukua mikoba ya Bologna mnamo Septemba baada ya kuondoka kwa Sinisa Mihajlovic na alionyesha kiwango kizuri katika mechi zake 32 za Serie A, na kupata wastani wa pointi 1.5 kwa kila mechi wakati huo akiwa na chapa nzuri ya soka.
Kama ilivyoripotiwa na kituo cha Ufaransa Foot Mercato, Bologna sasa wanatarajia kumpoteza Motta kwenda PSG na tayari wameanza kuandaa orodha ya makocha wanaoweza kuchukua nafasi.

Katika siku za hivi karibuni, majadiliano kati ya kocha na klabu kuhusu mipango ya soko la uhamisho wa majira ya joto yalivuruga uhusiano huo, na kocha huyo mwenye umri wa miaka 40 sasa anasubiri ofa rasmi kutoka kwa wababe hao wa Ligue 1.
Makocha watatu ambao kwa sasa wanafikiriwa na Bologna ni Luca Gotti, Gabriele Cioffi na Andrea Pirlo, huku Gennaro Gattuso na Igor Tudor pia wakiwa wagombea wanaowezekana.

