Klabu ya Simba imefikia uamuzi wa kumuajiri mtangazaji wa Clouds Media, Farhan Kiham kuwa Mkurugenzi wa Mashabiki wa klabu hiyo na mpango wa kumtangaza imeshakamilika na itafanyika muda wowote kuanzia sasa.
Taarifa zenye uhakika na bila chembe ya shaka zinaeleza kuwa Simba wanataka kumpa jukumu la kusajili wanachama wapya wa timu hiyo kwa njia ya mtandao kama ambavyo Yanga walivyofanikiwa kwa kipindi cha muda mfupi.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Mtoa taarifa alisema kuwa: “Simba imeamua kuboresha uongozi wake kwa upande wa mashabiki baada ya kuona wenzao Yanga wanafanikiwa kuvuna kipato kikubwa kwa upande wa mashabiki na ndiyo maana wameamua kumpa kazi hiyo Farhan.


