Ancelotti Akiri Kukoshwa Na Kiwango Cha Estevão

Kocha mkuu wa Brazil, Carlo Ancelotti, ameibua mjadala baada ya kutoa sifa nzito kwa kijana wa Chelsea, Estevão, kufuatia kiwango chake cha juu katika ushindi wa 2–0 dhidi ya Senegal kwenye uwanja wa Emirates. Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 18 aliendelea kung’ara kwa kufunga bao lake la nne katika mechi kumi tu za kikosi cha wakubwa cha Selecão.

Estevão amekuwa katika kiwango cha juu msimu huu akiwa na Chelsea, licha ya kutumika zaidi kama mchezaji wa kutokea benchi na kocha Enzo Maresca. Hata hivyo, kila mara anapopewa nafasi, ameonyesha ubora uliowafanya wengi wamuone kama nyota muhimu ya baadaye.

Ancelotti Akiri Kukoshwa Na Kiwango Cha Estevão

Kasi, utulivu, uwezo wa kumalizia na ubunifu wa kufungua mabeki vimeufanya ulimwengu wa soka kumtazama kama kipaji kipya kinachokuja kwa nguvu.

Baada ya mchezo dhidi ya Senegal, Ancelotti hakuacha nafasi ya mashaka kuhusu thamani ya kijana huyo.

“Estevão ana kipaji cha ajabu,” alisema. “Ana uwezo wa kumalizia, ana uwezo mkubwa na anafanya kazi kwa bidii sana. Kwa kumuangalia, naweza kusema Brazil ina uhakika wa siku zijazo.”

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Ancelotti aliyejenga majina makubwa kama Kaka, Benzema, Vinicius Jr na wengine, aliongeza kuwa kwa kiwango cha Estevão, muda mwingi hauhitajiki ili kuonyesha tofauti.

“Anaweza kuingia kwa dakika tano tu na bado akaonyesha ubora wake. Brazil ina bahati sana kuwa naye, na Chelsea pia.”

Ancelotti Akiri Kukoshwa Na Kiwango Cha Estevão

Kipaji cha Estevão kinatajwa kuwa miongoni mwa vipaji bora zaidi duniani kwa upande wa vijana, na thamani yake inaendelea kupanda. Ripoti zinaeleza kuwa Chelsea huenda wakalipa takribani pauni milioni 50 kumalizia masuala ya mikataba yake.

Hata hivyo, The Blues hawana presha ya kumkimbiza uwanjani kutokana na wingi wa vipaji eneo la ushambuliaji. Maresca tayari amekuwa akitoa nafasi kwa wachezaji kama Alejandro Garnacho, Pedro Neto na Jamie Gittens, huku mashabiki wakisubiri kurejea kwa Cole Palmer kutoka majeruhi.

Kwa kasi hii, ni wazi Estevão anajiandaa kuwa mmoja wa wachezaji muhimu zaidi wa Brazil chini ya Ancelotti kwenye Kombe la Dunia 2026 nchini Marekani, Canada na Mexico. Kiwango chake cha sasa kimewafanya mashabiki wa Brazil na Chelsea kuamini kwamba wanamiliki mmoja wa vipaji hatari zaidi vinavyokuja.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.