Mabingwa wa Euro 2016, Ureno, wametuma ujumbe mzito kwa wapinzani wao baada ya kuichapa Armenia 9–1 na kutinga Kombe la Dunia 2026 kwa kishindo. Wakati huo huo, Norway imeandika historia baada ya kufuzu kwa mara ya kwanza tangu 1998, ikiichapia Italia nyumbani kwao kwa ushindi wa mabao 4–1 katika uwanja wa San Siro.
Baada ya matokeo yasiyotabirika dhidi ya Hungary na kisha kipigo cha kushtusha kutoka Ireland, Ureno walihitaji ushindi wa uhakika na wakautoa kwa kiwango cha juu kabisa. Bila Cristiano Ronaldo aliyeapata kadi nyekundu mchezo uliopita, Bruno Fernandes na João Neves walibeba jukumu la ufungaji, kila mmoja akifunga hat-trick mbele ya mashabiki wa Porto.
Renato Veiga, Gonçalo Ramos na Francisco Conceição nao waliongeza ladha ya ushindi huo mnono.
Kwa mara ya saba mfululizo, Ureno wanajihakikishia nafasi kwenye fainali za Kombe la Dunia. lakini bado wakisubiri ndoto yao ya kulitwaa kwa mara ya kwanza.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Ireland Yaandika Hadithi Yake, Yaingia Playoffs kwa Dakika ya 96

Katika mchezo mwingine wa kuvutia, Troy Parrott aliingia kwenye vitabu vya historia vya Ireland kwa kufunga hat-trick ya dakika za majeruhi iliyowapeleka moja kwa moja kwenye hatua ya mchujo. Bao lake la mwisho, dakika ya 96, lilimgeuza shujaa wa taifa baada ya Ireland kutoka nyuma kwa mabao mawili dhidi ya Hungary.
Parrott, aliyeiumiza Ureno siku chache zilizopita, aliendeleza moto huo na kuwapa Ireland matumaini mapya kuelekea Machi.
Norway Yarejea Kwenye Ramani ya Dunia Baada ya Miaka 28



