Roma Wanashindana na Juventus Kumpata Beki wa Bournemouth, Federico Senesi.

Corriere dello Sport inaripoti kuwa Roma wako tayari kushindana na Juventus ili kumsajili beki wa AFC Bournemouth, Marcos Senesi, kama mchezaji huru mwezi Juni.

Roma Wanashindana na Juventus Kumpata Beki wa Bournemouth, Federico Senesi.

Beki huyo wa Bournemouth amevutia vilabu vya Serie A, Juventus na Roma.

Gazetta dello Sport iliripoti Ijumaa kuwa Bianconeri wako tayari kumpa beki huyo wa kati wa Argentina mkataba wenye thamani ya zaidi ya euro milioni 4 kwa msimu. Hata hivyo, kwa mujibu wa Corriere dello Sport, timu hiyo pia wanafuatilia kwa karibu hali ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27.

Gazeti hilo la jijini Roma limethibitisha kuwa Senesi hataongeza mkataba wake na Bournemouth, na ataondoka katika klabu hiyo ya England kama mchezaji huru mwishoni mwa msimu.

Hapo awali, Barcelona na Napoli walihusishwa na beki huyo wa Argentina, lakini sasa Roma na Juventus ndio vinatajwa kuwa wagombea wakuu wa kupata saini yake.

Roma Wanashindana na Juventus Kumpata Beki wa Bournemouth, Federico Senesi.

Juventus pia wanamvizia beki wa Roma, Zeki Çelik, ambaye anadaiwa kuhitaji euro milioni 4 kwa msimu ili kuongeza mkataba wake unaoelekea kuisha katika mji mkuu.

Juventus na timu hiyo  watakutana wiki ijayo katika dimba la Stadio Olimpico kwenye mechi muhimu katika mbio za kuwania nafasi ya kufuzu UEFA Champions League.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.