Mabingwa wa Kihistoria wa Ligi ya Tanzania Yanga imerejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo uliopigwa jana saa 10 katika Uwanja wa KMC Complex uliopo Mwenge Dar es Salaam.
Katika mchezo huo, mabingwa hao watetezi walionyesha ubora mkubwa kuanzia dakika za mwanzo hadi mwisho wa mchezo, ikitawala umiliki wa mpira na kutengeneza nafasi nyingi za mabao. Ushindi huo umeipa timu hiyo morali kubwa kuelekea michezo ijayo, hususan Kariakoo Derby inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki.
Mabao ya Yanga yalifungwa na Mohamed Hussein, Laurindo Dilson βDepuβ, Mudathir Yahya, Prince Dube na Sheikhan Khamis, kila mmoja akichangia kwa namna yake kuifanya timu hiyo iondoke na alama zote tatu muhimu.
Bila kusahauΒ meridianbetΒ ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa




