Nyota wa zamani wa Manchester United, Jesse Lingard, anaripotiwa kuwa katika mazungumzo ya hatua ya juu kujiunga na klabu ya Corinthians ya Brazil. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 33 yuko tayari kuanza changamoto mpya barani Amerika Kusini baada ya kuondoka FC Seoul mwishoni mwa mwaka jana.
Lingard aliachana na FC Seoul Desemba 2025 kwa makubaliano ya pande zote kuvunja mkataba, na tangu hapo amekuwa akitafuta timu mpya. Awali alihusishwa na vilabu kadhaa, ikiwemo Wrexham A.F.C. pamoja na uwezekano wa kurejea Ulaya, huku pia kukiwa na tetesi za kujiunga na Clube do Remo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa




