Felipe Luis Ahusishwa na Nafasi ya Ukocha Chelsea Baada ya Kufukuzwa Flamengo

Aliyekuwa kocha wa CR Flamengo, Felipe Luis, anaripotiwa kuwa miongoni mwa makocha wanaowania kuchukua nafasi ya ukocha katika Chelsea FC kufuatia kufutwa kazi kwake mapema mwezi Machi.

Felipe Luis Ahusishwa na Nafasi ya Ukocha Chelsea Baada ya Kufukuzwa FlamengoLuis mwenye umri wa miaka 40 alikuwa na kipindi cha mafanikio ndani ya Flamengo, akifanikiwa kushinda ubingwa wa ligi pamoja na taji la Copa Libertadores katika muda wake wa takribani mwaka mmoja na nusu.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Pamoja na mafanikio hayo, alifutwa kazi kwa kushangaza baada ya ushindi mkubwa wa mabao 8-0 dhidi ya Madureira RJ, huku ripoti zikidai kuwa sababu mojawapo ni mazungumzo aliyokuwa nayo na kampuni ya uwekezaji ya BlueCo inayohusishwa na Chelsea.

Felipe Luis Ahusishwa na Nafasi ya Ukocha Chelsea Baada ya Kufukuzwa Flamengo“Ilikuwa ni hali ya kushangaza sana. Nilidhani mazungumzo yalikuwa kwa nafasi kubwa zaidi, lakini baadaye nikagundua haikuwa hivyo,” alinukuliwa Luis akielezea hali hiyo.

Inaelezwa kuwa awali Luis aliamini kuwa alikuwa akizungumza kuhusu nafasi ya kuchukua mikoba ya Enzo Maresca, lakini baadaye akagundua mazungumzo hayo yalihusiana na klabu ya Strasbourg, jambo lililomfanya ajiondoe kwenye mchakato huo.

Felipe Luis Ahusishwa na Nafasi ya Ukocha Chelsea Baada ya Kufukuzwa Flamengo
Kwa sasa, Chelsea wanaendelea kutathmini chaguzi mbalimbali za makocha, huku majina ya Cesc Fabregas, Andoni Iraola na Marco Silva yakitajwa pia kuwania nafasi hiyo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.