Liverpool wamepiga hatua kukaribia kumsajili kiungo wa Brighton Alexis Mac Allister huku mwanahabari Gaston Edul akidai kuwa Jogoo wamepambana na ushindani kutoka kwa Chelsea kumpata mshindi huyo wa Kombe la Dunia.

Na gwiji wa taarifa za uhamisho Fabrizio Romano anaamini kuwa masharti ya kibinafsi yanakaribia kukubaliwa.
Hata hivyo, The Blues wanatumai kwamba uteuzi wa kocha wa Argentina Mauricio Pochettino unaweza kumshawishi raia wake kuchagua Stamford Bridge badala ya Anfield.
Kikwazo kingine kwa Merseysiders ni matarajio ya Mac Allister kucheza Ligi ya Mabingwa msimu ujao.

Sare ya 1-1 nyumbani na Aston Villa, pamoja na ushindi wa 1-0 wa Manchester United dhidi ya Bournemouth hapo jana kumekiacha kikosi hicho cha Jurgen Klopp kikiwa karibu kabisa kucheza Ligi ya Europa msimu ujao.
Lakini huku James Milner, Alex Oxlade-Chamberlain na Naby Keita wakiwa wamethibitishwa kuondoka katika klabu hiyo msimu huu wa joto, Klopp anatamani sana kuongeza usajili wa hali ya juu kwenye chumba chake cha injini.

Kwa upande wa Seagulls, mkufunzi Roberto De Zerbi amejiuzulu kwa kumpoteza nyota wake nambari 10 msimu huu wa joto lakini Football Insider inaripoti kwamba anatamani sana kuwashikilia Kaoru Mitoma na Moises Caicedo.

