Kama ilivyotarajiwa, Roma wametangaza mpango wa kumuuza Benjamin Tahirovic kwa Ajax na inaripotiwa wataweka mfukoni €8.5m pamoja na asilimia ya ada ya mauzo.

Kiungo huyo alifikisha umri wa miaka 20 mwezi Machi na tayari ana mechi tatu za wakubwa Bosnia na Herzegovina.
Iliripotiwa mapema leo kwamba makubaliano na Ajax yalikuwa karibu, licha ya nia kutoka kwa Olympique Marseille, Genoa, Sassuolo na Salernitana.
Hilo lilithibitishwa na taarifa kwenye tovuti rasmi ya klabu, ikibainisha kuwa uhamisho huo unasubiri kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.

Kulingana na mtaalam wa uhamisho wa Sky Sport Italia Gianluca Di Marzio, Roma wameweka masharti yatakayowaletea €8.5m kutokana na mauzo hayo, ikiwa ni pamoja na bonasi mbalimbali zinazohusiana na utendaji.
La Gazzetta dello Sport wanadai ni €5m pamoja na bonasi, ikijumuisha ada ya kuuza. Giallorossi pia wanawekeza katika mustakabali wa Tahirovic kwa kupunguzwa kwa asilimia 15 ya ada yoyote ya kuuza.
Alizaliwa na kukulia nchini Sweeden, akihama kutoka Vasalunds hadi akademia ya Roma kwa euro 204,000 tu mnamo Februari 2021.

Tahirovic alipandishwa kwenye kikosi cha wakubwa na Jose Mourinho, akicheza mechi 11 za Serie A na mbili kwenye Coppa Italia msimu huu.

