Kocha wa Juventus, Luciano Spalletti, ametoa kauli ya kushangaza na ya uaminifu mkubwa baada ya sare ya 1-1 dhidi ya Fiorentina, akisema wazi kuwa aliwaingiza David Openda na Jonathan David uwanjani kwa kuchelewa.

Kauli hii imezua mjadala mpana miongoni mwa mashabiki wa Juventus, hasa ikizingatiwa kuwa wawili hao ni miongoni mwa usajili muhimu wa dirisha la majira ya kiangazi.
Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Artemio Franchi, mashabiki wengi walitarajia kuona michango ya washambuliaji hao mapema, lakini Spalletti aliwaacha benchi hadi dakika ya 88, ambapo walichukua nafasi za Dusan Vlahovic na Kenan Yildiz. Hata hivyo, muda huo mdogo haukuwapa nafasi ya kufanya tofauti kubwa ndani ya mchezo.
Wakati wa mkutano na waandishi wa habari baada ya mchezo, mwandishi mmoja alimuuliza kwa nini hakuwatumia wachezaji hao mapema. Kwa unyenyekevu na uwazi.
Licha ya kuwa na matarajio makubwa, wachezaji hao wawili hawajaanza kutoa matokeo yaliyotarajiwa. Jonathan David hadi sasa amefunga bao moja na kutoa asisti moja katika mechi 15, huku Loïs Openda hajafunga kabisa katika msimu huu wa 2025-26. Hali hii imeongeza presha kwa Spalletti kuwapanga vizuri ili kuleta tija kwa timu.


