Kikosi cha Simba SC kimewasili visiwani Zanzibar kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Muungano Cup yaliyoanza rasmi Aprili 21, 2026, huku timu hiyo ikiwa na malengo makubwa ya kufanya vizuri katika michuano hiyo.
Simba wanatarajiwa kushuka dimbani kesho, Aprili 23, 2026, katika mchezo wao wa kwanza dhidi ya Mafunzo FC utakaopigwa majira ya saa 2:15 usiku kwenye Uwanja wa New Amaan Complex.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Mara baada ya kuwasili Zanzibar, kikosi cha simba kimeendelea na maandalizi ya mwisho kwa ajili ya mchezo huo, huku benchi la ufundi likihakikisha wachezaji wote wako katika hali nzuri ya ushindani.
Akizungumza baada ya kuwasili, kiungo mshambuliaji wa Simba, Neo Maema, amesema timu imejipanga vyema kwa ajili ya mashindano hayo na ipo tayari kupambana ili kufikia malengo waliyojiwekea.
Maema ameongeza kuwa lengo kubwa la Simba ni kutwaa ubingwa wa Muungano Cup, akisisitiza kuwa wataingia uwanjani kwa nidhamu, umakini na ari ya ushindi katika kila mchezo watakaocheza.

