Manzambi anaendelea kuwa na msimu mzuri wa kujitangaza akiwa na SC Freiburg, ambapo ameonyesha kiwango cha kuvutia tangu kupandishwa kikosi cha kwanza.
Kwa mujibu wa ripoti ya TEAMtalk, vigogo wa Premier League Arsenal, Chelsea na Manchester United wanaendelea kumfuatilia kwa karibu kiungo huyo kijana wa Freiburg kwa uwezekano wa kumsajili majira ya kiangazi.
Kiungo huyo wa kimataifa wa Switzerland ana msimu mzuri wa kujitambulisha katika Bundesliga, ambapo Freiburg kwa sasa wanashika nafasi ya nane kwenye ligi kuu ya Ujerumani.
Uchezaji wa Manzambi katikati ya uwanja haujapita bila kuonekana, kwani klabu hizo tatu za England zimeonyesha nia ya kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20.

Arsenal wanatarajiwa kuimarisha safu yao ya kiungo majira ya kiangazi na pia wamehusishwa na uwezekano wa kumsajili Leon Goretzka kutoka Bayern Munich.
Kwa upande wa Chelsea, wanatarajiwa kuweka kipaumbele katika nafasi hiyo wakati wa dirisha la usajili na wamekuwa wakionyesha mara kwa mara nia ya kuwasajili vipaji bora vijana barani Ulaya.
Wakati huo huo, Manchester United wanaaminika kuwa tayari wamemtazama Manzambi kupitia wapelelezi wao wa vipaji wakijiandaa kwa uwezekano wa kufanya uhamisho majira ya kiangazi.
Kama ilivyo kwa Chelsea, United pia wanatarajiwa kuimarisha eneo muhimu la kikosi chao mara dirisha la usajili litakapofunguliwa baadaye mwaka huu.
Casemiro anatarajiwa kuondoka Old Trafford mkataba wake wa sasa utakapoisha, huku mustakabali wa Manuel Ugarte katika klabu hiyo ukiwa bado haujulikani.
Si klabu za Arsena, Chelsea na United pekee zinazomfuatilia nyota huyo wa Freiburg. Bayern Munich na Bayer Leverkusen pia zinaripotiwa kufuatilia hali ya Manzambi.

Aidha, Paris Saint‑Germain na Napoli pia wanamchunguza kiungo huyo ambaye Freiburg wanamthamini kwa takribani pauni milioni 43 huku wakijaribu kuzuia klabu nyingine kumchukua mmoja wa wachezaji wao muhimu.
Klabu ya Galatasaray kutoka Turkish Süper Lig, ambayo hivi karibuni iliishinda Liverpool katika UEFA Champions League, pia imetajwa kuonyesha nia ya kumsajili kiungo huyo.
Kwa sasa SC Freiburg wana msimu usio thabiti, wakiwa nje ya mbio za kufuzu mashindano ya Ulaya lakini pia wako salama dhidi ya kushuka daraja.
Watakuwa wakitarajia kumaliza mfululizo wao wa mechi mbili bila ushindi watakapokutana na Union Berlin Jumapili mchana.