Lautaro Huenda Akakosa Dabi ya Milan Baada ya Inter Kuthibitisha Ukubwa wa Jeraha Lake.

Lautaro Martínez amepata majeraha ya kuvuta msuli (muscle strain) katika misuli ya soleus ya mguu wake wa kushoto. Jeraha hilo linatarajiwa kumuweka nje ya uwanja kwa takribani mwezi mmoja na linaweza kumkosesha dabi dhidi ya AC Milan.

Lautaro Huenda Akakosa Dabi ya Milan Baada ya Inter Kuthibitisha Ukubwa wa Jeraha Lake.

Inter walitoa taarifa rasmi jana kufuatia vipimo vya kitabibu vilivyofanywa asubuhi kwa mshambuliaji huyo.

Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina alipata maumivu ya misuli ya mguu (calf) wakati wa mechi ya UEFA Champions League dhidi ya Bodø/Glimt na alitolewa kipindi cha pili.

Inter walisema vipimo vilibaini kuwa ana “majeraha ya kuvuta msuli katika soleus ya mguu wake wa kushoto” na kwamba hali yake “itatathminiwa tena wiki ijayo.”

Kwa mujibu wa Sky Sport na Corriere dello Sport, Lautaro atalazimika kukaa nje kwa wiki tatu hadi nne, hali inayomaanisha atakosa dabi dhidi ya Milan itakayochezwa mwishoni mwa wiki ya Machi 8.

Lautaro Huenda Akakosa Dabi ya Milan Baada ya Inter Kuthibitisha Ukubwa wa Jeraha Lake.

Hata hivyo, Gazetta inaeleza kuwa Inter wana matumaini kuwa mfungaji wao bora msimu huu anaweza kurejea kwa wakati kabla ya dabi hiyo, ingawa atakosa mechi nne zijazo dhidi ya Lecce na Genoa katika Serie A, Bodø/Glimt katika Ligi ya Mabingwa, pamoja na Como kwenye Coppa Italia.

Msimu huu, Lautaro Martínez amefunga mabao 18 na kutoa pasi nne za mabao katika mechi 35 kwenye mashindano yote.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.