Lautaro Martinez ameisifu Inter Milan kwa ujasiri wao mkubwa baada ya kuiondoa Bayern Munich na kufuzu kwa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Barcelona. “Hatukati tamaa, tuna kichwa na moyo,” alisema mshambuliaji huyo wa Argentina.

Mchuano huo ulikuwa wa ushindani mkubwa katika mechi zote mbili, lakini ushindi wa 2-1 jijini Munich uliwapa faida Inter, kwani sare ya 2-2 kwenye uwanja wa San Siro usiku wa jana ilitosha kuwapa tiketi ya kusonga mbele.
Harry Kane alifungua mabao kwa shuti kali la pembeni lililoibua shambulizi la ghafla kutoka Inter, ambao walijibu ndani ya dakika tisa kupitia mabao ya Lautaro Martinez na Benjamin Pavard yaliyoanzia kona.
Eric Dier alifunga bao la kusawazisha kwa kichwa kutoka pembeni kwa mtindo wa kipekee, lakini Inter walihimili presha hadi dakika ya mwisho na sasa watakutana na Barcelona katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa.
“Bila shaka ilikuwa mechi ya kipekee na ya kukumbukwa kwa muda mrefu, kwa sababu Inter ina nyoyo kubwa. Kuna kazi kubwa sana na kujitolea katika hatua hii ya kufuzu. Hatukati tamaa, tuna kichwa na moyo. Ni kweli, tuliteseka katika baadhi ya vipindi vya mchezo, lakini tunaweza kulenga mafanikio makubwa.” alisema Lautaro Martinez kupitia Amazon Prime Video Italia.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.



