Kipa wa Manchester City James Trafford amekuwa akipata changamoto ya kupata nafasi ya kucheza mara kwa mara kufuatia ujio wa Gianluigi Donnarumma msimu uliopita wa joto hivyo uhamisho wa kwenda Aston Villa ndio changuo la kwanza.

James Trafford amehusishwa na uwezekano wa kuondoka Manchester City msimu huu wa joto. Aston Villa wanamnyatia kipa huyo wa Manchester City kama mbadala wa Emiliano Martínez, kulingana na The Daily Mail.
Trafford alirejea Manchester City msimu uliopita akiwa na matumaini ya kuwa kipa namba moja baada ya kufanya vizuri akiwa Burnley msimu uliopita.
Hata hivyo, City waliamua kumsajili Gianluigi Donnarumma siku ya mwisho ya dirisha la usajili, jambo lililomfanya Trafford kupata nafasi ndogo sana ya kucheza.
Kipa huyo wa Uingereza hajaanza mechi ya ligi tangu kipigo cha 2-1 dhidi ya Brighton mwezi Agosti na amekuwa akitumika kama mchezaji wa akiba.
Hata hivyo, amekuwa akifanya vizuri anapopewa nafasi, akisaidia City kushinda mechi za kombe dhidi ya Arsenal na Liverpool.

Ingawa Manchester City hawako tayari kumuuza kirahisi, Trafford anataka kucheza mara kwa mara, hivyo uhamisho wa majira ya joto unaonekana kuwa uwezekano mkubwa. Aston Villa ni miongoni mwa klabu zinazomfuatilia kwa karibu.
Kwa upande wa Emiliano Martínez, amekuwa akihusishwa na uwezekano wa kuondoka Villa Park baada ya pia kujaribu kuondoka msimu uliopita.
Jaribio lake la kujiunga na Manchester United halikufanikiwa, na pia Atletico Madrid walionyesha nia, lakini bado ameendelea kuwa chaguo la kwanza chini ya Unai Emery.
Villa wanapima uwezekano wa kumuuza mchezaji huyo ili kupunguza mzigo wa mishahara, kwani ni miongoni mwa wanaolipwa zaidi klabuni.


