Manchester United wako tayari kushindana na Chelsea pamoja na klabu ya Serie A Juventus katika kinyang’anyiro cha kumsajili nyota wa Lens Mamadou Sangare, kulingana na taarifa za Calciomercato.

Manchester United wanatarajiwa kuimarisha kiungo chao msimu huu wa joto, huku Sangare akiibuka kama lengo muhimu kwa kikosi cha Michael Carrick.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 amekuwa mhimili muhimu wa Lens msimu huu, huku klabu hiyo ikiendelea kufanya vizuri na kushangaza wengi katika mbio za ubingwa.
Lens wakiwa chini ya kocha Pierre Sage wako pointi nne nyuma ya vinara Paris Saint-Germain, ingawa wamecheza mechi moja zaidi. Timu hiyo inaweza kupunguza pengo hadi pointi moja iwapo watashinda dhidi ya Toulouse Ijumaa usiku.
Fomu nzuri ya Sangare imevuta macho, akiwa mmoja wa wachezaji bora wa Lens katika msimu wa 2025–26 ikiwemo Manchester.


