Klabu ya Mbeya City FC imetangaza rasmi kusitisha mkataba na kocha wake mkuu, Mecky Maxime, pamoja na benchi lake la ufundi, kufuatia makubaliano ya pande zote mbili.
Uamuzi huo umetolewa kupitia taarifa rasmi ya klabu hiyo kwa umma, ukieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuleta mabadiliko ndani ya timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya NBC.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Hatua hiyo imekuja muda mfupi baada ya Mbeya City kupokea kipigo kizito cha mabao 6-0 kutoka kwa mabingwa watetezi Yanga. Matokeo hayo yameonekana kuwa kichocheo kikubwa cha mabadiliko hayo.
Katika taarifa yake, uongozi wa klabu ulieleza kuwa, “Tumefikia makubaliano ya kusitisha mkataba na Kocha Mecky Maxime pamoja na wasaidizi wake. Tunatambua na kuthamini jitihada walizozifanya katika kipindi chote walichokuwa nasi.” Kauli hiyo inaonesha kuwa licha ya matokeo mabaya ya hivi karibuni, mchango wa benchi la ufundi umetambuliwa.
Aidha, klabu hiyo iliongeza kwa kusema, “Tunamshukuru Kocha Maxime kwa mchango wake na tunamtakia kila la kheri katika hatua zake zijazo.” Wasaidizi walioguswa na uamuzi huo ni pamoja na kocha msaidizi Nizar Khalfa na kocha wa viungo Francis Mkanula, ambao nao wameondoka sambamba na kocha mkuu.Kwa sasa, Mbeya City FC inatarajiwa kuanza mchakato wa kutafuta kocha mpya atakayechukua nafasi hiyo, huku lengo likiwa ni kurejesha ushindani ndani ya ligi kuu ya NBC.

