Mbio za ubingwa wa La Liga zimechukua sura mpya nje ya uwanja baada ya Kamati ya Waamuzi ya Hispania (CTA) kukiri rasmi kuwa bao la ushindi lililofungwa dhidi ya FC Barcelona halikupaswa kusimama. Katika kipigo cha kushtukiza cha mabao 2-1 dhidi ya Girona FC Februari 16 kwenye Uwanja wa Montilivi, Fran Beltran alifunga bao la dakika ya 86 lililozua hasira kubwa kwa Wacatalunya.




