Monaco wamejiweka katika nafasi nzuri katika kinyang’anyiro cha kumsajili kiungo wa Juventus Denis Zakaria baada ya uamuzi wa West Ham kuzingatia malengo mengine.

The Hammers walikuwa kwenye mazungumzo na Bianconeri kuhusiana na dili la mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 lakini walishindwa kupata makubaliano, huku kusisitiza kwao kwa mkataba wa mkopo na kusababisha mazungumzo kugonga kizuizi.
Odds kubwa kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti ni vitu vinavyoweza kubadilisha maisha yako kwa kukupatia pesa nyingi. Ingia mchezoni hapa.
Zakaria ameondolewa kwenye mradi wa Juventus na hakujiunga na kikosi kwa ajili ya ziara ya kujiandaa na msimu mpya nchini Marekani, badala yake alibaki Turin akisubiri kujua mustakabali wake.

Kama ilivyoangaziwa na Calciomercato.com, Monaco wanataka kumnunua Zakaria msimu huu wa joto na wako kwenye mazungumzo na msafara wa kiungo huyo wa Juventus. Ofa inaweza kutumwa katika siku zijazo.
Tembelea duka la ubashiri-Meridianbet kutandika jamvi lako kwa odds kubwa.
Bianconeri wanataka angalau €20m kwa mchezaji huyo, ambaye ana kandarasi ya kuitumikia klabu hiyo hadi Juni 2026. Alitumia msimu uliopita kwa mkopo na Chelsea, lakini alitatizika kupata muda wa kucheza mara kwa mara, akipata dakika 599 tu za kucheza.

