Ligi kuu ya NBC Tanzania Bara kuendelea hii leo kwa michezo miwili ambapo mchezo wa mapema ni huu unaowakutanisha kati ya Singida Big Stars dhidi ya Polisi Tanzania majira ya saa 10:00 jioni.

Mchezo huo utapigwa katika dimba la Liti huku timu hiyo ya Pluijm ikiwania nafasi nne bora za juu kabla ya ligi kuu haijamalizika ambapo mpaka sasa Singida anashikilia nafasi ya 3 akiwa na pointi zake 48 akiwa ameshinda mechi zake 14, sare 6, na kupoteza mara 5.
Wakati Polisi Tanzania bado hali mbaya sana kwenye msimamo wa ligi akiwa nafasi ya mwisho baada ya kukusanya pointi zao 19, akishinda mechi zake 4, sare 7 na kupoteza mara 14.

Walima alizeti wanaitaka nafasi ya tatu halikadhalika, Polisi Tanzania nao bado wanataka kupata ushindi lakini je wataweza mbele ya vijana wa Pluijm ambao wanaonekana kuwa na ubora kabisa.

