Beki wa Manchester United, Harry Maguire, amemsifu kocha Michael Carrick kwa kuibadilisha timu hiyo na kuirejesha kwenye ushindani, kufuatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Brentford F.C.
Ushindi huo umeifanya United kukaribia kufuzu kwa UEFA Champions League msimu ujao, ikiwa ni mabadiliko makubwa ukilinganisha na msimu uliopita walipomaliza nafasi ya 15.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Michael Carrick alichukua nafasi ya Ruben Amorim mwezi Januari baada ya kipindi kigumu, ambapo wachezaji walikuwa wanapata shida kuendana na mbinu za kocha huyo wa zamani.
Akizungumza baada ya mchezo, Maguire alisema, “Tulianza na mechi ngumu dhidi ya Arsenal na Man City, lakini tuliweza kupata pointi sita muhimu, jambo lililoongeza imani kwa kila mmoja ndani ya timu.”
Aliongeza, “Tangu kocha mpya aingie, matokeo yanaonyesha kila kitu. Tumeimarika zaidi katika safu ya ulinzi na ushambuliaji, na sasa tuna uwezo wa kufunga mabao kutoka sehemu yoyote.”
Manchester United kwa sasa wapo nafasi ya tatu wakiwa na pointi 61, na ushindi tisa katika mechi 13 chini ya Carrick umeiweka timu hiyo katika nafasi nzuri ya kurejea kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

