Ni kutokana na Chelsea kucheza Jumatatu usiku ndiyo maana mechi yao dhidi ya Tottenham Hotspur huenda isihamishiwe kwenye wiki ya kati ya Mei 4–10.
“The Blues” kisha watarudi kwenye majukumu ya EPL Jumamosi, Mei 9 watakapokwenda kucheza ugenini dhidi ya Liverpool katika dimba la Anfield.
Spurs nao watakutana na Leeds United katika raundi hiyo hiyo ya mechi Jumatatu, Mei 11 katika Tottenham Hotspur Stadium. Kutokana na ratiba hiyo, pia hakuna uwezekano wa kutumia katikati ya wiki hiyo kwa mechi ya Tottenham dhidi ya Chelsea.
Chelsea kisha watacheza na Manchester City katika fainali ya FA Cup Mei 16, na ni baada ya tarehe hiyo ndipo Spurs wanaweza kutarajia kukutana na The Blues.

Kwa hivyo, mechi kati ya Chelsea na Tottenham ina uwezekano mkubwa kupangwa katika wiki inayofuata baada ya fainali ya FA Cup na kabla ya siku ya mwisho ya msimu wa EPL Mei 24.
Hii ingemaanisha Tottenham Hotspur kucheza dhidi ya Chelsea katikati ya wiki, kisha kukutana na Everton katika mechi yao ya mwisho ya ligi msimu huu.
Kwa upande wa Chelsea, hii ingemaanisha The Blues kucheza dhidi ya Manchester City kwenye fainali ya FA Cup, kisha mechi iliyopangwa upya dhidi ya Tottenham Hotspur, na hatimaye kufunga msimu wa EPL dhidi ya Sunderland zote ndani ya wiki moja.