Roy Hodgson anadai Crystal Palace imesalia kwenye pambano la kushushwa daraja lakini kazi inayowakabili si kubwa sana baada ya kuambulia pointi 10 katika mechi nne zilizopita.

Palace walishinda mechi zao tatu za kwanza chini ya Hodgson kufuatia mwendo wa bila ushindi wa michezo 12 huku bosi wa zamani Patrick Vieira akiwa ameshika usukani. Sare tasa ya Jumamosi nyumbani dhidi ya Everton iliongeza mwendo na kuwaacha vijana wa Hodgson kwa pointi tisa zaidi ya eneo la kushuka.
The Eagles bado wanamkosa Wilfried Zaha kutokana na jeraha la paja na nyota wao atakosa kucheza tena usiku wa kuamkia leo katika uwanja wa Wolves.
Hodgson mwenye miaka 75, alisema: “Nadhani saizi ya kupigana tunayepigana inaweza kuwa ndogo kidogo. Bado ni vita, hakuna shaka juu ya hilo. Sitafikia hatua ya kuongelea usalama wa kimahesabu. Bado nadhani timu yoyote yenye pointi 37 ambayo imekaa nyuma na kufikiria kuwa kazi iliyofanyika inafanya makosa makubwa.”

Hodgson amesema kuwa itakuwa ukosefu wa ajabu wa tamaa na taaluma na hamu ya kuwa na michezo sita mbele yako na kuamua kuwa pointi 37 zitawasaidia. Alisema pia alienda pale kwa matumaini na ikitokea kwamba wako pale klwa pointi 37 na tofauti ya mabao na iwe hivyo.
Alipoulizwa kama Zaha atarejea kwenye timu, Roy aliongeza: “Jibu la uaminifu ni kwamba Wilf anapokuwa fiti atacheza, bado nadhani mtu atakuwa tegemezi kwa wachezaji wake bora, na mchezaji anayeshinda mechi lakini ili kuwa timu nzuri unahitaji zaidi ya bao moja.”

Palace wanaweza kuipita Chelsea hadi nafasi ya 11 kwa ushindi dhidi ya Molineux, jambo ambalo lilionekana kutofikirika Roy aliporejea Machi 21. Kwenye hatua hiyo, pengo la The Blues lilisimama kwa pointi 11 lakini Palace sasa wako nyuma kwa pointi mbili pekee.

