Chelsea haijalishi kama Romelu Lukaku atahamia Inter msimu huu wa joto. Muda tu akiondoka kwenye klabu, kulingana na ripoti mbalimbali Italia.

Chelsea ambayo ni ya London Magharibi wanataka tu kumuuza Lukaku na mkataba wa mkopo haupo mezani. Klabu inataka kuhifadhi nafasi zake za mkopo kwa ajili ya kutuma wachezaji wachanga kusaidia maendeleo yao.
Kuhusu Lukaku, The Blues wangependa kumuuza kabla hawajaondoka kwa ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya nchini Marekani siku ya Jumapili.
Inter wamekuwa kwenye mazungumzo na Chelsea kuhusu mpango wa kumnunua Mbelgiji huyo kwa kitita cha euro milioni 35-€40.

The Nerazzurri wameripotiwa kusubiri hadi uhamisho wa Andre Onana kwenda Manchester United ukamilike kabla ya kuweza kuilipa Chelsea ada wanayotaka.
Lukaku mwenyewe pia ameweka wazi kuwa hana nia ya kuungana na wachezaji wenzake wa Chelsea kwa kutorejea kwa ajili ya mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya pamoja na wachezaji wengine wa kikosi hicho wiki iliyopita.
Lakini, ripoti za jana jioni zilionyesha kwamba mpango huo ulikwama kwa sababu hakuna klabu ambacho kimeweza kuwasiliana na wakili wa Lukaku, Sebastien Ledure, ambaye amekuwa akihusika sana katika mazungumzo.

Huku Mauricio Pochettino ameamua kwamba Lukaku si sehemu ya mipango yake ya msimu wa 20223-24, La Gazzetta inaandika kwamba Chelsea haijalishi ni wapi Lukaku atacheza soka lake msimu ujao, mradi tu aondoke kwenye klabu hiyo majira ya joto, kabla ya Jumapili.

