Klabu ya KMC imeshindwa kufurukuta hapo jana baada ya kuchezea kichapo cha mabao 5-0 dhidi ya Yanga katika dimba la Chamazi majira ya saa 1:00 jioni.

KMC alikuwa ugenini baada ya mechi ya kwanza ya ligi kutoa sare akiwa ugenini pia dhidi ya Namungo lakini sare ile ilikuwa ya kufungana bao 1-1.
Wakati huo huo Yanga ndio mechi yao ya kwanza na wameanza vizuri kwa kufunga mabao mengi huku yakifungwa na wachezaji mbalimbali akiwemo Aziz Ki, Konkoni, Job, Mudathir, Pacome.

Vijana wa Moallini walizidiwa kila kitu kwenye mchezo huo kuanzia eneo la mbele, ulinzi na kiungo huku mashbiki wakimsifu mwalimu Gamondi kwa kuibadilisha klabu hiyo ya kuwa inafunga magoli mengi.
Wanakino Boys wanahitaji kujipanga zaidi baada ya msimu uliopita kuangukia Pla-off na hatimaye kuweza kusalia kwenye Ligi. Je msimu huu watashika namba gani?

