Aston Villa wanapima uwezekano wa kufanya uhamisho mkubwa majira ya kiangazi kwa ajili ya nyota wa Nottingham Forest, Morgan Gibbs-White, kwa mujibu wa TEAMtalk.

Gibbs-White alikuwa karibu kujiunga na Tottenham mwaka jana baada ya Spurs kuamilisha kipengele cha kuachiliwa (release clause) kilichokuwa kwenye mkataba wa kiungo huyo.
Ofa hiyo ilisababisha hasira kubwa kutoka kwa Forest, ambao walifikiria kuchukua hatua za kisheria dhidi ya klabu hiyo ya kaskazini mwa London.
Hatimaye, Gibbs-White alisaini mkataba mpya na The Tricky Trees, lakini tetesi kuhusu mustakabali wake zimeendelea kushika kasi. Forest wanapitia msimu mgumu na kwa sasa wapo pointi mbili tu juu ya eneo la kushuka daraja kufuatia michezo ya Jumanne.
Hata hivyo,klabu hiyo imemtimua Sean Dyche, ambaye ni kocha wa tatu wa Forest msimu huu, Villa wanaripotiwa kufuatilia kwa karibu hali ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26.
The Villans walijaribu kusajili kiungo mpya dirisha la Januari kufuatia majeraha ya Boubacar Kamara na Youri Tielemans.
Kikosi cha Unai Emery kilionekana kuwa karibu kumsajili Conor Gallagher kutoka Atletico Madrid, lakini kiungo huyo wa Uingereza aliishia kujiunga na Spurs.


