Tuchel Asaini Mkataba Mpya na Uingereza Hadi Euro 2028

Thomas Tuchel amesaini mkataba mpya na timu ya taifa ya Uingereza utakaodumu hadi pale michuano ya Euro 2028 itakapofika.

Tuchel Asaini Mkataba Mpya na Uingereza Hadi Euro 2028

Kocha huyo Mjerumani alichukua mikoba ya kuinoa Three Lions Januari mwaka jana na aliiongoza Uingereza kufuzu Kombe la Dunia 2026 kwa rekodi ya asilimia 100, baada ya kushinda mechi zote nane alizosimamia.

Mkataba wa awali wa Tuchel ulikuwa umepangwa kumalizika baada ya mashindano hayo ya kiangazi, lakini sasa amekubali kuongeza muda wake wa kuinoa timu hiyo kwa miaka miwili zaidi.

“Thomas Tuchel amesaini mkataba mpya wa kuiongoza timu ya wakubwa ya wanaume ya Uingereza hadi UEFA EURO 2028 nchini Uingereza na Ireland,” ilisoma taarifa kwenye tovuti ya Shirikisho la Soka la Uingereza.

Baada ya kuiongoza Three Lions bila kupoteza katika kampeni ya kufuzu iliyovunja rekodi kwa ajili ya Kombe la Dunia lijalo la FIFA litakalofanyika Canada, Mexico na Marekani, Tuchel amekubali kubaki kama kocha mkuu kwa miaka miwili zaidi.

Uingereza hawakufungwa bao hata moja katika kampeni hiyo ya mafanikio, wakifunga mabao 20, na wameendelea kubaki miongoni mwa timu tano bora duniani kwa miaka saba na nusu sasa.

Tuchel Asaini Mkataba Mpya na Uingereza Hadi Euro 2028

Alipoulizwa anajisikiaje kusaini kwa miaka miwili zaidi, Tuchel alisema: “Nina furaha sana. Mwanzoni nilitaka mkataba wa muda mfupi wa miezi 18 tu kwa sababu sikuwa na uhakika nini kitanisubiri katika soka la kimataifa; nitaweza kuzoea kwa haraka kiasi gani na kazi hii inahusu nini hasa?

Tuchel alisema kuwa mapema sana aliipenda kazi hii na nafasi hii, na tangu siku ya kwanza alijitoa kikamilifu na alijivunia sana.

“Sasa, katika miezi sita iliyopita hasa kwa kile tunachokijenga, ari inayokua na kuunda uhusiano wa kipekee kati ya wachezaji pamoja na matokeo mazuri sana, ni furaha kuongeza mkataba na kujaribu kukamilisha mzunguko kamili wa mashindano mawili.”

Uingereza watacheza dhidi ya Uruguay na Japan katika dirisha la kwanza la mechi za kimataifa la mwaka ujao mwezi ujao. Baadaye, Three Lions watakutana na New Zealand na Costa Rica kabla ya Kombe la Dunia 2026, ambapo wamepangwa kundi moja na Croatia, Ghana na Panama.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.