Chelsea Wamefungua Uwezekano wa Kumuza Alejandro Garnacho Chini ya Mwaka 1 Tangu Kumsajili.

Chelsea wanataka kumuuza Alejandro Garnacho chini ya mwaka mmoja tangu walipomsajili kutoka Manchester United, kwa mujibu wa talkSPORT.

Chelsea Wamefungua Uwezekano wa Kumuza Alejandro Garnacho Chini ya Mwaka 1 Tangu Kumsajili.

Maisha ya Garnacho ndani ya Manchester United yaliharibika baada ya kauli zake hadharani kuhusu nafasi yake katika fainali ya UEFA Europa League. Kufuatia hilo, aliyekuwa kocha wakati huo Ruben Amorim anaripotiwa kumwambia kuwa afadhali aombe apate klabu ya kumsajili.

Chelsea walikuwa wakimfuatilia kwa muda na hatimaye walimsajili kwa pauni milioni 40, lakini mshambuliaji huyo wa pembeni hajafikia matarajio ya thamani yake, akiwa amefunga bao moja tu na kutoa pasi nne za mabao katika EPL msimu huu.

Kwa mujibu wa talkSPORT, Chelsea sasa wako tayari kumuuza Garnacho, wakifikia uamuzi huo chini ya mwaka mmoja tangu ajiunge na klabu hiyo. Inaelezwa pia kuwa uongozi wa klabu unakubaliana kwamba dili hilo halijaenda kama ilivyotarajiwa.

Hakuna taarifa rasmi ya bei ambayo klabu ya Stamford Bridge itakubali kwa sasa, lakini kutokana na kiwango chake kushuka, huenda wakalazimika kumuuza kwa bei ya chini kuliko waliyonunulia.

Chelsea Wamefungua Uwezekano wa Kumuza Alejandro Garnacho Chini ya Mwaka 1 Tangu Kumsajili.

Ripoti nyingine zinaeleza kuwa Anthony Gordon anapangwa kuwa mbadala wa Garnacho katika nafasi ya winga wa kushoto Chelsea.

Garnacho pia amekosolewa vikali na baadhi ya wadau wa soka. Nguli wa Manchester United Nicky Butt alimkosoa kwa tabia yake wakati alipokuwa Old Trafford, akisema licha ya uwezo wake, mtazamo wake haukuwa mzuri.

Kwa upande mwingine, mwandishi wa Daily Star Jeremy Cross alimshambulia kwa kusema kuwa Garnacho ni mfano wa wachezaji wa kisasa wenye kujiamini kupita kiasi kuliko uwezo wao, akidai ana kiburi na kujiona kupita kiasi.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.