Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Tottenham Hotspur, Christian Eriksen, amesema anaamini klabu hiyo ina ubora wa kutosha kuendelea kubaki kwenye Ligi Kuu ya England licha ya kupambana na hatari ya kushuka daraja msimu huu.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Denmark, ambaye alikuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya Spurs ikiwemo kufika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2019, amesema inaumiza kuona timu yake ya zamani ikiwa katika hali ngumu. Eriksen alikuwa mhimili mkubwa katika enzi ya mafanikio chini ya kocha Mauricio Pochettino kati ya mwaka 2014 hadi 2019.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Katika kipindi chake Spurs kuanzia 2013 hadi 2020, Eriksen alicheza jumla ya mechi 305, akifunga mabao 69 na kutoa pasi za mabao 88. Pia alitwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Klabu mara mbili na kujumuishwa kwenye Kikosi Bora cha Professional Footballers’ Association msimu wa 2017/18.
Akizungumza na Viaplay, Eriksen ambaye kwa sasa anachezea VfL Wolfsburg na kupambana pia kuepuka kushuka daraja kwenye Bundesliga, alisema hali ya Spurs inamuumiza lakini bado ana matumaini watanusurika.
“Inauma kutazama ukiwa nje. Inakera. Natumaini watafanikiwa kubaki kwa sababu klabu kama Tottenham lazima icheze Ligi Kuu ya England. Hilo ni la uhakika,” alisema Eriksen.
Aliongeza: “Itakuwa jambo la kusisimua kuona kama wataweza. Ninaendelea kuwaombea na kutumaini watafanikiwa. Ni wazuri sana kushuka daraja, lakini hivyo ndivyo unavyosema kwa karibu timu zote zinazoshuka. Hata hivyo, ukitazama mchezaji mmoja mmoja, ni wazuri mno kushuka daraja.”
Kwa sasa, Tottenham wana alama 31 baada ya kucheza mechi 33 na wanashika nafasi ya chini wakibaki pointi mbili nyuma ya West Ham United walio juu kidogo ya mstari wa kushuka daraja. Wakati Burnley na Wolverhampton Wanderers tayari wameshuka, Spurs wanaendelea kupambana kusalia na mechi tano zilizobaki msimu huu.

