Mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Tanzania bara msimu wa 2021/22 Yanick Bangala amesajiliwa na mabingwa wa Tanzania bara msimu wa 2013/2014 klabu ya Azam FC.
Bangala ambaye pamoja na mwenzie Djuma Shaban hawako kwenye mipango ya Yanga msimu huu kiasi hawakuwa sehemu ya utambulisho wa wachezaji waliotambulishwa kwenye kilele cha wiki ya Mwananchi kilichofanyika tarehe 22.Julai. 2023.
Beti na Meridianbet kwa odds kubwa na machaguo kibao, pia unaweza kubashiri mubashara.
Habari za uhakika kutoka kwenye chanzo cha kuaminika kinasema Yanga watapokea Tshs100M kwa biashara hii.
Bangala na Djuma wameigomea Yanga kwenda kwa mkopo Singida Fontain Gate baada ya kutokea mgogoro wa kimkataba na nafasi zao kuzibwa na Yao Yao na Pacome.
Azam itaondoa mchezaji mmoja wa kimataifa ili kumpa Bangala nafasi huku Azam wakitakiwa kumaliza biashara hii haraka.
Odds kubwa kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti ni vitu vinavyoweza kubadilisha maisha yako kwa kukupatia pesa nyingi. Ingia mchezoni hapa.