Kocha mkuu wa Juventus Massimiliano Allegri amethibitisha kuwa Angel Di Maria atapatikana kwa mechi ya kesho dhidi ya Lecce, lakini Adrien Rabiot na Alex Sandro huenda wakapumzika.

Bianconeri watawakaribisha Lecce kwenye Uwanja wa Allianz siku ya kesho saa 17:00 kwa saa za Uingereza. Vijana wa Allegri wamepoteza mechi tatu na sare katika mechi nne zilizopita za Serie A na wamefunga mabao matatu pekee katika michezo sita iliyopita katika mashindano yote.
Di Maria hakupatikana katika mchezo wa Jumapili wa sare ya 1-1 dhidi ya Bologna Uwanja wa Stadio Dall’Ara kutokana na jeraha la kifundo cha mguu, lakini ripoti nchini Italia zilisema El Fideo alikataa kusafiri na timu kwa sababu alijua hangeanza.
Allegri amesema; “Di Maria anajisikia vizuri, hasikii tena maumivu kwenye kifundo cha mguu na kesho anaweza kuhusika Tunatarajia mengi kutoka kwake na kwa wengine. Bila shaka, Di Maria anaweza kuleta mabadiliko katika mchezo.”

Allegri anatarajiwa kucheza kwa kupokezana dhidi ya Lecce kwani Bibi Kikongwe atacheza mechi tatu ndani ya wiki moja na mechi mbili za Serie A na mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya Ligi ya Europa dhidi ya Sevilla mnamo Mei 11.
Kocha huyo amekiri kuwa Rabiot alicheza vyema Bologna, lakini pengine atapumzika katika mechi inayofuata. Bremer alihitaji kupumzika dhidi ya Bologna. Huu ni msimu wa kwanza anacheza mchezo kila baada ya siku tatu. Sio rahisi kila wakati, lakini kesho atarudi. Nadhani Alex Sandro atapumzika dhidi ya Lecce kwa sababu amecheza sana kwa hivyo tunahitaji nguvu mpya.
Juventus walipata ushindi wa 1-0 katika mchezo wa mchujo uliochezwa kwenye Uwanja wa Stadio Via Del Mare huku Nicolò Fagioli akifunga la ushindi na bao lake la kwanza kwa timu ya wakubwa ya Bianconeri.

Allegri alipoulizwa kuhusu maendelea ya kiungo huyo alisema kuwa lazima aimarike, kama mchezaji yeyote wa soka. Kila mchezaji wa mpira wa miguu lazima afanye kazi ili kuboresha hadi mwisho wa kazi yake. Fagioli ameimarika sana. Na ansema kuwa alimbadilisha dhidi ya Bologna si kwa sababu alistahili, lakini kwa sababu alihitaji wachezaji wenye sifa tofauti. Alikuwa amecheza mchezo mzuri.
Juventus ilishinda mechi mbili pekee mwezi Aprili, kwa hivyo Allegri anaelezeaje kiwango duni kama hicho.

Mkutano na waandishi wa habari ulimalizika kwa swali kuhusu Manuel Locatelli, ambaye amekuwa na hali ya juu na ya chini katika muhula huu: “Alicheza mchezo mzuri sana huko Bologna. Kisha, wachezaji hawawezi kuwa katika ubora wao katika kila mchezo. Manuel huwa anapatikana kwa timu, hata wakati hana siku nzuri kiufundi, kwa kujilinda yuko kila wakati.”

