Kocha wa timu ya Brighton De Zerbi amesema kuwa anadhani kuwa kwasasa hahitaji kusajili mshambuliaji katika dirisha dogo la usajili linalotarajiwa kufunguliwa mwezi Januari.

Aliongeza kwa kusema kuwa wachezaji wake Danny Welbeck na Leandro Trossard wako imara na wako tayari kucheza katika eneo la ushambuliaji hivyo hana wasiwasi katika eneo hilo.
De Zerbi alijiunga na Brighton siku si nyingi akichukua mikoba ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo Graham Potter na kuhamia Chelsea, ambapo kocha huyo ameshinda mechi yake ya pili mfululizo ndani ya Uingereza.

Kocha huyo amesema kuwa mwezi Januari anahitaji zaidi kusajili beki mpya wa kati ili waweze kujiimarisha katika eneo lao la ulinzi kutokana na kuruhusu sana mabao ambapo hapo jana wameshinda dhidi ya Wolves kwa mabao 3-2, na kuwafanya wasogee hadi nafasi ya 6.

Ulishawahi kuwaza kuwa rubani wa maisha yako!! Kuwa rubani wa mchezo pendwa wa Aviator wa kasino mtandaoni. Aviator bonanza inazidi kutoa michongo ya mkwanja kwenye nyumba ya mabingwa. Unarusha ndege yako na unashinda, kuwa rubani wa kujivunia kwa kuibuka na mkwanja leo.
BONYEZA HAPA

