KAPOMBE AFUNGUKA ISHU YA KUWATOA TMA

Shomari Kapombe beki wa Simba amesema kuwa walikutana na ushindani mkubwa kutoka kwa wapinzani wao TMA Stars katika mchezo wa hatua ya 32 bora CRDB Federation Cup uliochezwa Uwanja wa KMC Complex.

KAPOMBE AFUNGUKA ISHU YA KUWATOA TMA

Katika mchezo huo uliochezwa Machi 11 2025 baada ya dakika 90 ubao ulisoma Simba 3-0 TMA Stars kwa mabao ya Valentin Nouma dakika ya 15, Sixtus Sabilo alijifunga dakika ya 19 na Leonel Ateba alifunga bao la tatu dakika ya 75.

Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Kwenye mchezo huo nyota Sabilo dakika ya 45 alifanya jaribio la hatari ambalo lilimpa tabu kipa namba mbili wa Simba, Ally Salim ambaye alikuwa langoni kwenye mchezo huo likiwa ni jaribio pekee lililokuwa na hatari zaidi kwa upande wa TMA Stars.

KAPOMBE AFUNGUKA ISHU YA KUWATOA TMA

Kapombe ameweka wazi kuwa waliingia kwa malengo yakupata ushindi kwenye mchezo huo jambo ambalo lilifanikiwa baada ya mchezo kukamilika.

“Ilikuwa ni mechi yenye ushindani mkubwa hasa ukizingatia kwamba hatua ya mtoano kila timu inatafuta ushindi, kushinda kwetu ni furaha na tunaamini kwamba tutaendelea kupambana kupata matokeo mazuri kwenye mechi zijazo.” Alisema Kapombe.

Simba inatinga hatua ya 16 bora inaungana na Yanga ambayo ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Coastal Union ya Tanga, Uwanja wa KMC Complex Machi 12 2025.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.