Pep Guardiola anaamini kwamba Manchester City sasa wanapaswa kushinda kila mchezo ili wawe na nafasi ya kuwashinda Arsenal na kutwaa ubingwa wa EPL.

Manchester City wataendeleza harakati zao za kuwafukuzia Arsenal walio kileleni mwa msimamo watakapomenyana na Chelsea Jumapili, baada ya mapumziko ya takribani mwezi mmoja kutokana na mechi za kimataifa na mashindano ya kombe.
Hata hivyo, hata wakipata pointi zote kwenye mechi zao zilizosalia nane ikiwa ni pamoja na mchezo wa nyumbani dhidi ya Arsenal wiki ijayokikosi cha Guardiola bado kitahitaji vinara hao kupoteza pointi ili kuwa na nafasi ya kutwaa taji.
Kocha wa Manchester City alisema: “Hali tuliyonayo katika EPL, tunahitaji kushinda mechi zote vinginevyo haitatupa nafasi ya kupigania ubingwa hadi mwisho. Tunahitaji kukusanya pointi nyingi. Hatukuwa na uthabiti wa kutosha na katika msimu tulipoteza pointi ambazo tulipaswa kuzipata. Ndiyo maana tuko katika nafasi ambayo sasa hatuwezi kufanya tofauti.”
Manchester City wanaelekea Stamford Bridge wakiwa na morali nzuri baada ya kushinda Carabao Cup kwa ushindi wa kujiamini dhidi ya Arsenal, kisha kuicharaza Liverpool mabao 4-0 kwenye FA Cup.
Arsenal watacheza kabla yao mwishoni mwa wiki hii, lakini Guardiola alisisitiza kuwa hilo halibadili chochote kwenye mtazamo wa City.

Alisema: “Tunahitaji kushinda mechi zetu, iwe tunacheza kabla au baada. Sasa kuna mechi chache zilizobaki katika EPL, hivyo lazima tushinde kila moja.”
Manchester City wanaonekana kuwa na morali nzuri na pia watajipa moyo kutokana na rekodi yao nzuri ya mwezi Aprili, wakiwa wameshinda mechi 28 kati ya 31 walizocheza katika mwezi huo.
Hata hivyo, kocha Pep Guardiola hatoi uzito mkubwa sana kwenye takwimu hizo.
Alisema: “Nimepokea kadi nyingi za njano, hiyo inaonyesha jinsi ninavyokuwa na hisia kali. Sio tu mwezi Aprili, msimu mzima nimekuwa na nguvu nzuri na bado nina nguvu hiyo.”
Manchester City bado wanakabiliwa na changamoto za ulinzi, huku Rúben Dias akiwa nje kutokana na majeraha, John Stones akipimwa utimamu wake wa afya, na Josko Gvardiol akiwa majeruhi wa muda mrefu.

