Sassuolo wamepata dili la kumnunua kiungo wa kati wa Valencia na Serbia Uros Racic ambaye atafanyiwa vipimo vyake kesho.

Kulingana na Sky Sport Italia, atasafiri kwa ndege jioni hii na kuwa tayari kufanya majaribio kesho asubuhi.
Odds kubwa kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti ni vitu vinavyoweza kubadilisha maisha yako kwa kukupatia pesa nyingi. Ingia mchezoni hapa.
Inaaminika kuwa ni uhamisho wa gharama ya takriban €2.5m, ada ya chini ikizingatiwa kuwa mkataba wake unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu. Racic amekubali mkataba wa miaka mitatu na Neroverdi.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ameichezea Serbia mara 11 na alicheza kwa mkopo Ureno msimu uliopita akiwa na SC Braga.

Uzoefu wake wa awali wa mkopo ni pamoja na Famalicao na Tenerife, wakati alipitia akademi ya vijana ya Red Star Belgrade.
Tembelea duka la ubashiri-Meridianbet kutandika jamvi lako kwa odds kubwa.

