Kwa mujibu wa vyanzo vya karibu na Mqatar huyo, Sheikh Jassim bado anasubiri kusikia iwapo ofa yake ya tano na ya mwisho kwa Manchester United imefanikiwa.

Ripoti za hivi majuzi ndani ya Qatar zilisema kwamba ofa ya Sheikh ambayo ni ya asilimia 100 ya klabu ilishindwa na mwanzilishi wa Ineos Sir Jim Ratcliffe.
Hata hivyo, kambi ya Sheikh Jassim ilizitaja ripoti hizo kuwa ni uvumi mtupu na kusema zimesalia katika mfumo wa kushikilia. Wanatarajia hatua inayofuata itakuwa kwa bodi ya United kukutana na kuzingatia ofa zote mbili.
Ofa ya tano ya Sheikh Jassim ilitolewa wiki iliyopita, lakini wakati huo huo iliwekwa wazi kwa familia ya Glazer ambao wanamiliki klabu na kwa kikundi cha benki cha wafanyabiashara cha Raine ambacho kinasimamia uuzaji kwamba hatajihusisha na mchakato huo zaidi ya mwisho.

Raia hao wa Qatar wana hamu ya kukamilisha dili hilo huku dirisha la usajili la majira ya kiangazi likikaribia kuanza. Ofa ya Sheikh Jassim inafahamika kuwa ni mkataba wa pesa taslimu kwa asilimia 100 ya klabu, na kwamba madeni yote ya United yatafutwa.
Vyanzo vilivyo karibu na ofa ya Sheikh vinasema kwamba fedha tofauti, za ziada zitapatikana kwa ajili ya kuajiri wachezaji, miundombinu na mahitaji mengine ya uwekezaji.
The Glazers walitangaza kwa mara ya kwanza nia yao ya kufikiria kuuzwa kwa klabu mnamo Novemba mwaka jana, na ofa za kwanza kutoka kwa Ratcliffe na Sheikh Jassim ziliwasilishwa mnamo Februari.

Kumekuwa na ripoti kwamba ofa ya Ratcliffe ni ya asilimia 60 ya klabu, huku Avram na Joel Glazer wakibakiza asilimia 20 ya hisa, lakini vyanzo vya karibu na Ratcliffe havijathibitisha hili.

