Endrick amefichua Vinicius Junior na Cristiano Ronaldo walishiriki katika uamuzi wake wa kujiunga na Real Madrid.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 16 amekubali kujiunga na LaLiga na mabingwa wa Ulaya Madrid kutoka Palmeiras mnamo Julai 2024.
Endrick alikuwa akihusishwa na vilabu kama Paris Saint-Germain na Chelsea kabla ya kuamua kuhamia jiji hilo kuu la Uhispania kwa mkataba ambao unaweza kugharimu €70milioni.

Mchezaji mwenzake wa Brazil Vinicius na mfungaji bora wa muda wote wa Madrid, Ronaldo walishawishi uamuzi wa kijana kuhamia Los Blancos.
Aliiambia Marca: “Real Madrid ni timu kubwa sana, na Vini alikuwa amenitumia ujumbe na kunipa matumaini zaidi.
“Cristiano, ambaye ni mchezaji ninayempenda sana, pia aliichezea Real Madrid. Ndiyo maana nilichagua Real Madrid na nadhani ni chaguo sahihi. Mungu amekuwa nami siku zote na ameniambia kuwa hiyo ndiyo njia bora zaidi.”

Carlo Ancelotti pia alimshawishi Endrick kwamba kujiunga na Madrid lilikuwa chaguo lake bora zaidi, akiongeza kuwa alizungumza na kocha wa timu hiyo, na Rodrygo pamoja na Wder Militao, na Wabrazil.
Endrick anamshukuru Mungu sana kwa kila kitu kinachotokea katika maisha yake na anatumai kuwa mengi mazuri bado yanakuja, lakini anapaswa kuweka miguu yake chini, kuwa na unyenyekevu na uvumilivu.

