Klabu ya Yanga imeishikisha adabu timu ya Rhino Rangers hapo jana katika dimba la Mkapa baada ya kuitandika kwa mabao 7-0 kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam.

Mchezo huo ulipigwa jana majira ya saa 1:00 usiku huku mpaka kufikia dakika 45 za kwanza za mchezo, Yanga walikuwa tayari wanaongoza kwa mabao 5 kwa bila huku Kennedy Musonda naye akiingia kambani.
Mabao hayo ya Young Africans yalitupiwa kimyani na Ambundo, Bangala, Aziz Ki, Faridi mussa, Musonda mabao mawili na Bryson na kukamilisha jumla ya idadi ya mabao saba huku Rhino Rangers wakigalagazwa vibaya.

Timu hiyo inayoshiriki Ligi daraja la pili, walishindwa kufanya chochote kutokana na kuzidiwa na Mabingwa hao watetezi wa Kombe hili.

