Klabu ya Simba itavuna 5.8 Bilioni kwenye maandalizi tuu ya michuano ya CAF Super Cup huku CAF tayari ikiwa imeshateua timu nane ambazo zitashiriki michuano hii kwa mara ya kwanza Afrika.

Simba ndio timu pekee inayoshiriki michuano hii Tanzania, lakini pia Afrika Mashariki na Kati baada ya kuwa ana mwendelezo wa kufanya vizuri kwenye michuano ya klabu bingwa anayoshiriki karibu kila mwaka.
Timu zingine kutoka Afrika zinazoshiriki michuano hii ya Super Cup ni pamoja na Al Ahly kutoka Misri, Raja Casablanca, Wydad Casablanca kutoka Morocco, Horoya kutoka Guinea, Hearts of Oak kutoka Ghana, Mamelod Sundowns kutoka Afrika Kusini, ES Tunis kutoka Tunisia ambazo jumla zinafika timu 8.

Lakini pia taarifa zinasema kuwa CAF wanaangalia kama kuna uwezekano wa kuongeza timu nne zaidi, ili kufanya ligi hiyo kuwa na timu 12 huku michuano hiyo ikitarajiwa kuanza mwaka huu mwezi wa nane.

