Ronaldo Afunga Bao la Kwanza la Al Nassr Jana

Cristiano Ronaldo alifunga bao lake la kwanza kwa Al Nassr na kuipatia timu yake pointi moja dhidi ya Al Fateh siku ya jana.

 

Ronaldo Afunga Bao la Kwanza la Al Nassr Jana

Nahodha huyo wa Ureno, ambaye alihamia Saudi Arabia kama mchezaji huru alifungua akaunti yake kwa kupachika bao la penalti ya dakika za lala salama katika Uwanja wa Prince Abdullah bin Jalawi.

Vinara hao wa Saudi Pro League Al Nassr walitoka nyuma mara mbili na kupata pointi moja ugenini.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 37 alipiga mkwaju wake kwa utulivu dakika ya 92 kabla ya mchezaji mwenzake Talisca, ambaye alifunga bao la kwanza la Al Nassr kufuta bao la kuongoza la Cristian Tello, kutolewa nje kwa kadi nyekundu katika mchezo wa mwisho.

Ronaldo Afunga Bao la Kwanza la Al Nassr Jana

Ronaldo alikuwa ameifungia Riyadh All-Stars mabao mawili katika sare ya 5-4 ya kirafiki dhidi ya Paris Saint-Germain iliyojumuisha Lionel Messi na Kylian Mbappe mwezi uliopita.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.