Afisa Habari wa klabu ya Yanga, Ali Kamwe amethibitisha mchezaji wao Bernard Morrison atakuwa nje kwa muda wa miezi miwili baada ya kupata majeraha ya nyonga.

Mchezaji huyo ambaye ametoka kuonywa kutokana na kuchelewa kurudi kambini baada ya ligi kusimama kwaajili ya kupisha michuano ya Mapinduzi yaliyokuwa yanafanyika kule Zanzibar atakosa michezo ya awali ya makundi ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya US Monastir ya Tunisia February 12.
Uwepo wa Morrison kwenye kikosi cha Nabi ilikuwa inamfanya kocha huyo kuwa na washambuliaji wengi kwenye eneo hilo la mbele ambalo linaongozwa na Fiston Mayele mwenye mabao 15.

Licha ya kutangazwa kuwa ameumia mchezaji huyo hajacheza mechi kadhaa za mabingwa hao watetezi wa ligi kuu msimu uliopita, na bado anaendelea kuwa nje tena kutokana na majeraha hivyo inawezekana ikawa ni pigo kwa kocha mkuu wa kikosi cha Yanga.

