Klabu ya Manchester City ina mpango wa kumnunua James Maddison huku dirisha la uhamisho likiwa limefungwa lakini uvumi bado umejaa huku vilabu vikifanya mipango yao ya kuongeza wachezaji katika msimu wa joto.

Kwa mujibu wa gazeti la The Daily Mail, Manchester City wanapanga kumsajili kiungo huyo wa kati ambaye ataweza kuwasaidia katika eneo hilo.
Mchezaji huyo wa Kimataifa wa Uingereza amekuwa akikabiliwa na tetesi nyingi za uhamisho katika kipindi cha miezi 12 iliyopita, huku klabu za Newcastle na Manchester United zikiwa zimetawala vichwa vya habari.
Wakati Foxes wamefanikiwa kumbakiza nyota wao kwa miezi michache zaidi, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ataingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake katika msimu wa joto.

Maddison amefunga mara saba kwenye Primia Ligi mwaka huu na ripoti zinaonyesha kuwa anaweza kuwa mbadala wa Bernardo Silva, ambaye anahusishwa kuondoka klabuni hapo.
Ilkay Gundogan ni mwingine ambaye anaweza kuondoka Etihad na hii ingempa Pep Guardiola tatizo kwenye kiungo ambalo linahitaji kushughulikiwa.
Ripoti hiyo inadokeza kwamba mabingwa hao wameuliza kuhusu kupatikana kwa mchezaji huyo wa Kimataifa mwenye mechi moja, huku timu hiyo ya East Midlands ikitaka ada kubwa ili kumwachilia.

City hawakutumia pesa nyingi katika soko la Januari lakini wangetafuta kujenga upya kikosi chao kilichogawanyika msimu wa joto badala yake.

