Kevin De Bruyne amefichua kuwa alikuwa na jeraha katika kipindi chote cha mwisho cha ushindi wa Manchester City wa Treble.

De Bruyne hakuwa uwanjani wakati City ilipomaliza msimu mzuri kwa kushinda Ligi ya Mabingwa siku ya Jumamosi, baada ya kushindwa na tatizo la msuli wa paja la muda mrefu.
Mchezaji huyo wa Ubelgiji alilazimika kutolewa nje baada ya dakika 35 za mchezo mgumu wa fainali dhidi ya Inter Milan mjini Istanbul, ambapo City waliendelea kushinda 1-0 kwa bao lililofungwa na Rodri dakika ya 68.
De Bruyne alisema: “Ninatoa kila kitu kwa ajili ya timu yangu na watu katika klabu wanajua hilo. Ninajisikia fahari kwamba nimeweza kufanya nilichofanya. Ni aibu kwamba ilienda kama ilivyotokea kwangu hapa, lakini tunaenda kushinda Ligi ya Mabingwa kwa hivyo hakuna kitu kibaya kwake.”

Nilijisikia sawa wiki hii, lakini nimeambiwa kwa miezi miwili ilikuwa hatari lakini, unajua, unaikubali. Nilifanya nilichopaswa kufanya. Ni wazi nilikosa baadhi ya michezo lakini michezo kama Arsenal, Bayern Munich na Real Madrid nilifanikiwa kufanya hivyo. Alisema kiungo huyo.
“Nilikuwa na mambo ya kibinafsi kutokea na familia yangu juu ya hilo na niliweza hilo, lakini, hapa, mshipa wa paja ulikatika.”
Ilikuwa ni mara ya pili kwa mchezaji huyo kulazimishwa kutolewa nje katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kupata jeraha baya usoni walipopoteza dhidi ya Chelsea miaka miwili iliyopita.

Hata hivyo baada ya City kupita, hakutaka kuangazia masaibu yake binafsi akisema kuwa haangalii soka kwa njia hiyo alihisi timu ilikuwa na uwezo wa kuisimamia na kufanya kazi yao. Anasema kuwa jeraha sio zuri lakini alikuwepo kwaajili ya timu yake na alifanya kile alichohitajika kufanya.
“Nilijisikia sawa katika dakika 35 nilizocheza na siwezi kutarajia zaidi kutoka kwangu.”
Ushindi ulitimiza matarajio ya muda mrefu kwa Kevin baada ya kufurahia mafanikio makubwa ndani ya miaka nane aliyoitumikia City. Na kimsingi amekuwa akipigania maisha yake yote na timu yake kushinda medali hiyo.
Mengi yamefanywa kuhusu ushindi huo unaweza kumaanisha nini kwa City, kama jukwaa la timu ya sasa na hadhi ya klabu kwa ujumla, lakini Kevin anahisi hilo ni suala la siku nyingine.

Alisema: “Hilo si jambo ninalofikiria sana hivi sasa. Msimu ni mrefu sana tunapaswa kufurahia tu wakati huu. Tumekuwa na karamu ndogo hadi sasa, lakini sasa tunaweza kufurahiya sana kwa siku kadhaa, kama tunavyopaswa. Hatujapoteza mchezo hata mmoja katika Ligi ya Mabingwa msimu huu kwa hivyo nadhani tunastahili.”

