Liverpool Haiko Tayari Kumwachia Chiesa Hadi Wapate Mshambuliaji Mpya.

Liverpool hawako tayari kumuuza Federico Chiesa hadi pale Alexander Isak atakapowasili kutoka Newcastle United, kwa mujibu wa ripoti, hali inayowaacha Inter Milan na Napoli wakisubiri.

Liverpool Haiko Tayari Kumwachia Chiesa Hadi Wapate Mshambuliaji Mpya.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Italia alionekana kuwa njiani kuondoka zikiwa zimepita mwaka mmoja tu tangu ajiunge na Anfield akitokea Juventus, huku mkataba wake wa awali ukiwa unakaribia kwisha.

Hata hivyo, katika msimu wake wa kwanza, Chiesa hakucheza sana kutokana na majeraha au kiwango duni, ingawa aliweza kufunga mabao mawili na kutoa pasi mbili za mabao katika mechi 14 za mashindano rasmi.

Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Alipoachwa nje ya kikosi cha Liverpool kilichosafiri kwa ajili ya mechi za kirafiki za maandalizi ya msimu, wengi walidhani atatolewa kwa mkopo au kuuzwa.

Liverpool Haiko Tayari Kumwachia Chiesa Hadi Wapate Mshambuliaji Mpya.

Hata hivyo, La Gazzetta dello Sport inaripoti kuwa kocha Arne Slot wa Liverpool anataka kumbakisha Chiesa, angalau hadi pale watakapomsajili mshambuliaji mpya – huku lengo kuu likiwa ni nyota wa Newcastle United, Alexander Isak.

Inter Milan na Napoli bado wana nia ya kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27, huku Atalanta pia wakiwa waliwahi kuhusishwa, lakini hatua yoyote ya uhamisho italazimika kusubiri kwa sasa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.