Kwa mujibu wa Tuttosport, mapokezi mabaya ambayo Alessandro Bastoni amekuwa akipata katika viwanja vya Italia yanaweza kumshawishi mchezaji huyo wa kimataifa wa Italy kufikiria uhamisho kwenda Barcelona, ingawa Inter Milan hawako tayari kumuachia beki huyo kwa chini ya €70m.

Ripoti hiyo inaongeza kuwa Inter hawana nia ya kuuza nyota wao wa ulinzi Bastoni, ingawa Nerazzurri wanaweza kuvutiwa na ofa zitakazofikia karibu €70m, kulingana na taarifa za Tuttosport.
Gazeti hilo la Italia linadai kuwa kwa sasa wala Inter Milan wala beki wao Alessandro Bastoni hawafikirii kuachana majira ya kiangazi, lakini hilo halimaanishi kwamba Barcelona hawana matumaini ya kumsajili.
Kwa kweli, Inter wanaweza kukubali kusikiliza ofa zitakazofikia takribani €70m, huku Bastoni pia akishawishika kuondoka mwishoni mwa msimu, hasa baada ya mapokezi yasiyo mazuri aliyopata katika viwanja mbalimbali vya Italia katika wiki za hivi karibuni.
Mashabiki katika viwanja mbalimbali kote Italy bado wanamlenga mchezaji huyo wa kimataifa wa Italia, Alessandro Bastoni, kufuatia tukio lililosababisha Pierre Kalulu kupewa kadi nyekundu katika mechi ya Serie A kati ya Inter Milan na Juventus mwezi Februari.


