Kuna ripoti zinazoongezeka kuhusu nia ya Tottenham Hotspur kumtaka kocha Roberto De Zerbi, lakini kocha huyo wa Kiitaliano anatarajiwa kusubiri hadi majira ya joto kabla ya kukubali kazi mpya.

Kocha wa zamani wa Sassuolo na Brighton & Hove Albion, De Zerbi, anaweza kurejea kwenye Premier League majira ya joto, kwani anaripotiwa kuwa miongoni mwa majina makuu yanayozingatiwa kwa ajili ya kuinoa Tottenham.
Ben Jacobs ameripoti kupitia mtandao wa X kwamba: “Roberto De Zerbi kwa sasa anaelekea kusubiri hadi majira ya joto kabla ya kukubali kazi mpya, akijua kuwa klabu kadhaa zinamvutia. Kocha huyo wa Italia ni miongoni mwa majina yanayoongoza kwenye orodha fupi ya Tottenham Hotspur pamoja na Mauricio Pochettino.”
Mtaalamu huyo wa masuala ya uhamisho wa wachezaji pia ameongeza kuwa Tottenham wanatarajiwa kuachana na kocha Igor Tudor mwezi huu, huku klabu hiyo ya Kaskazini mwa London ikiwa inachunguza kwa makini uwezekano wa kupata kocha wa muda pamoja na kama wanaweza kuharakisha uteuzi wa kocha wa kudumu.
De Zerbi aliachana na Olympique de Marseille kwa makubaliano ya pande zote mwezi Februari, na ripoti za awali pia zilimhusisha na kazi ya kuifundisha Manchester United.


