Chelsea Wanamuwania Nick Woltemade

Chelsea wanaweza kumuachia Liam Delap huku wakimsajili Nick Woltemade kutoka Newcastle United. Kiwango cha mchezaji huyo kimepungua baada ya mwanzo mzuri aliokuwa nao.

Chelsea Wanamuwania Nick Woltemade

Kwa mujibu wa mdadisi Simon Phillips, Chelsea wanamuwania mshambuliaji wa Newcastle, Woltemade, na wanaweza kujaribu dili la kubadilishana wachezaji likimhusisha Delap, ambaye anaripotiwa kuwa tayari kuondoka Stamford Bridge.

Woltemade na Delap wote walihama klabu majira ya joto yaliyopita, ambapo Mjerumani huyo alijiunga na Newcastle akitokea VfB Stuttgart, huku Delap akihamia Chelsea kutoka Ipswich Town.

Woltemade alianza kwa kasi, akifunga mabao saba katika mechi 10 za kwanza za Premier League, lakini hajafunga tena tangu Desemba.

Kwa upande mwingine, Delap amekuwa chaguo la pili kwenye safu ya ushambuliaji ya Chelsea nyuma ya Joao Pedro, akiwa na bao moja tu la ligi. Ripoti zimekuwa zikieleza kuwa huenda akaondoka ndani ya mwaka huu, na sasa inaonekana ameona ni bora kuondoka.

Chelsea Wanamuwania Nick Woltemade

Hali hiyo inaweza kuipa Chelsea faida, kwani wanataka kumsajili Woltemade, huku Newcastle nao wakionekana kumtaka Delap, baada ya kumfuatilia tangu majira ya joto.

Inaripotiwa kuwa Chelsea watawasilisha ombi la kumtaka Woltemade ikiwa Newcastle wataonyesha nia ya kumsajili Delap, jambo ambalo linaweza kusababisha makubaliano ya kubadilishana wachezaji kati ya klabu hizo mbili za Premier League.

The Blues wako tayari kumpa Woltemade nafasi ya kucheza kama mshambuliaji namba 9 msimu ujao, licha ya uwepo wa João Pedro na ujio unaotarajiwa wa Emmanuel Emegha.

Awali, Woltemade alianza msimu akicheza kama mshambuliaji wa kati Newcastle, lakini hivi karibuni amehamishiwa zaidi nafasi ya kiungo mshambuliaji ili kuongeza mchango wake baada ya mabao kupungua.

Chelsea Wanamuwania Nick Woltemade

Hata hivyo, Woltemade sio chaguo pekee kwa Chelsea, kwani pia wanamuwania Julián Álvarez wa Atlético Madrid. Inaripotiwa kuwa Arsenal na FC Barcelona pia wanamuwania, jambo linaloweza kufanya dili hilo kuwa gumu kwa Chelsea.

Álvarez, ambaye alihusika moja kwa moja katika mabao 55 ndani ya mechi 103 akiwa Manchester City ameendelea kung’ara Hispania, akiwa na mabao 17 na asisti tisa msimu huu katika mashindano yote.

Pia ana uwezo wa kucheza nafasi tofauti za ushambuliaji, jambo linalompa The Blues chaguo zaidi, tofauti na Woltemade ambaye, licha ya kucheza nafasi ya kiungo mshambuliaji, bado hajafikia kiwango cha juu kama Álvarez katika majukumu hayo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.