Klabu ya RC Lens imekataa ombi la Paris Saint-Germain la kuahirisha mchezo wao wa ligi, uamuzi unaoongeza presha kwa PSG katika kipindi hiki chenye ratiba ngumu. PSG walikuwa wameomba mechi hiyo isogezwe mbele kutokana na kubanwa na michezo miwili muhimu dhidi ya Liverpool FC kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Taarifa zinaeleza kuwa Lens hawakuwa tayari kurahisisha hali kwa wapinzani wao, wakizingatia ushindani mkali uliopo kwenye msimamo wa ligi. Tofauti ya pointi kati ya timu hizo ni ndogo sana, hali inayofanya kila mchezo kuwa na uzito mkubwa katika mbio za ubingwa.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Hatua hiyo inaifanya mechi hiyo kuwa muhimu zaidi kwa pande zote mbili, huku PSG wakilazimika kupanga kikosi chao kwa umakini mkubwa ili kuhimili ushindani wa ndani na wa kimataifa kwa wakati mmoja.
PSG kabla ya kukutana na Lens tarehe 11 April atakuwa na mchezo dhidi ya Toulouse kwenye ligi 1 tarehe Aril 3 na mchezo wa robo fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya Liverpool siku ya tarehe 8 April.
Kwa upande wao, Lens wanaonekana kutumia fursa hiyo kuongeza presha kwa PSG, wakiamini kuwa ratiba hiyo ngumu inaweza kuwaathiri wapinzani wao katika mbio za ubingwa wa ligi.

