Pongezi kwa kila mtu aliyehusika katika miaka hiyo migumu, hasa Mark Robins, bila shaka anastahili kutajwa. Lakini huu ni mafanikio makubwa sana kwa kila aliyehusika na ni jambo la kipekee kweli. Nakosa maneno, na imekuwa ya hisia sana.
“Nilitaka tufanikishe hili tukiwa ugenini kwa kiasi fulani. Najua ilivyo kufanya hivi, hasa kwa mashabiki wanaosafiri kila mara kuisapoti timu ugenini ni mashabiki wa kujitolea sana na wanapata usiku wa maisha yao. Hii ndiyo sababu tunafanya kazi hii.” Alisema Lampard.
Kuhusu shamrashamra za ajabu mwishoni mwa mechi ambapo wachezaji, benchi la ufundi na hata mmiliki Doug King walijiunga kusherehekea na kupiga ‘fist pump’, kocha mkuu Frank Lampard alisema: “Ndiyo, nilikuwa nasubiri mtu afanye fist pump isiyovutia zaidi kuliko yangu, na Doug akaifanya! Inapendeza sana, na Doug anastahili kuwa katikati ya jukwaa kwa sababu yeye ndiye kiongozi mkuu wa klabu.”
Gazeti la Coventry Telegraph limetoa toleo maalum la kurasa 48 kuadhimisha mafanikio ya Frank Lampard na kikosi chake. Toleo hilo linajumuisha ripoti za mechi, picha, na maoni kutoka kila hatua ya safari ya kurejea kwenye ligi kuu ya Uingereza.
Tangu kushuka daraja mwaka 2001, “Sky Blues” wamepitia vipindi vigumu vilivyoandikwa sana, lakini baada ya robo karne, wamefanikiwa kupanda daraja kwa mtindo wa kuvutia. Pia kutakuwa na uchambuzi wa kina kuhusu msimu wa ubingwa, mafanikio ya Lampard, wachezaji muhimu, na nini kinawasubiri klabu hiyo katika ligi kuu.
Mwanahistoria wa klabu Jim Brown pia atatoa tathmini yake yenye takwimu kuhusu kupanda daraja, huku kukiwa na picha na ripoti za sherehe za furaha za mashabiki wa “Sky Blues”.
“Yeye ana shauku kubwa sana kwa hili na amefanya kazi kubwa kuifikisha klabu ilipo sasa. Kila mchezaji katika kikosi hiki kilichosimama uwanjani amechangia kwa namna fulani, na naweza kukaa hapa nikazungumzia kila mmoja wao kwa sababu nimewaona. Hatuko mbali sana na kundi lile lile lililokusanyika tulipowasili, mnamo Novemba na Desemba mwaka uliopita, na wamefanya kazi kwa bidii, wameendelea kuwa pamoja na wanacheza soka la kiwango cha juu sana mwaka huu.”
Wamedroo mechi tatu hivi karibuni na tayari wamepanda daraja huku zikiwa zimesalia mechi tatu. Hiyo inaonyesha uimara na uthabiti wa timu hii pamoja na namna ilivyofanikiwa, ambayo ni ya kipekee sana.
Anafikiri Ipswich Town waliwahi kufanya kitu kama hiko miaka michache iliyopita katika mazingira yao. Lakini wao walivyotoka karibu na mkia wa msimamo na ndani ya miezi mitano wakafika nusu fainali za play-off, halafu wakasema wataendelea tena na kuwa timu inayotawala ligi hiyo ni sifa kwa kazi ya kila mtu aliyehusika.